Posts

Showing posts from August, 2013

HOW TO BECOME A GOOD SINGER AND FAMOUS SINGER

HOW TO BECOME A GOOD AND FAMOUS SINGER   How To Improve Your Singing Voice. Want to learn how to improve your singing voice? First you have to know what you sound like when you sing. What you hear in your head is not how you really sound to others. You hear your own voice from the inside of your head, but others hear the sound waves leave your mouth and enter their ear drums. If you really want to know what you sound like, you'll have to listen to yourself outside of your head, then you can begin learning how to improve your singing voice. The best way to do this is of course to record yourself. The first time you hear yourself sing from a recording, you will probably deny that that is what your voice sounds like. Your voice will be different than what you thought it was from hearing it within your head. However, you have to accept that fact in order for you to be able to improve your singing voice. When you sing,

NJIA ZA KUPATA UTAJIRI WA KUDUMU

Image
MBINU ZA KUPATA UTAJIRI WA KUDUMU   BILA shaka ukiulizwa leo kama unataka kuwa tajiri, jibu lako litakuwa ni NDIYO! Lakini je, tunaelewa maana ya utajiri na namna ya kuwa tajiri? Hili ni swali ambalo majibu yake yanawasumbua wengi. Mada hii itakusaidia kupata mwanga wa maana na namna ya kuutafuta utajiri. Wengi wanaamini kuwa ili mtu awe tajiri lazima awe na bahati ya kipekee. Watu wengi hudhani kuwa hawawezi kuwa matajiri mpaka watumie mizizi ya Bagamoyo, Tanga au Sumbawanga. Wengine huamini kwamba ili uwe tajiri, ni lazima uoe au uolewe na tajiri. Zipo imani nyingi juu ya utajiri, wengine wanaamini lazima uwe na ‘zali’, ufanye biashara ya magendo, ukwepe kodi, uibe, utoe uhai wa mtu au utumie njia nyingine haramu ndiyo uupate utajiri.   SIRI YA UTAJIRI HII HAPA Siri kubwa ya mtu kuufikia utajiri wa kweli na wa kudumu, ni kuanzisha biashara yenye faida ambayo utakuwa na uwezo wa kuimiliki na siyo biashara ikumiliki wewe. Ukifanikiwa kuanzisha biashara yako, jambo la

HASARA YA CHUMVI

Image
HASARA YA CHUMVI Stori kuhusu chumvi: Tunapata chumvi nyingi kwenye vyakula vyetu siku hizi. Chumvi nyingi itasababisha shinikizo la damu, uvimbe, matatizo kwenye kibofu cha mkojo, matatizo ya moyo na orodha inaendelea. Tunaambiwa chakula chenye chumvi kidogo au kisicho na chumvi kabisa ndicho bora kwa afya zetu. Ukweli kuhusu chumvi: Mpaka zama za pili za mawe (middle stone ages), hakuna chumvi iliyokuwa mbaya. Waharifu waliuliwa gerezani kwa kupewa chakula bila chumvi, iliwasababishia kifo cha taratibu. Miaka 2000 iliyopita, chumvi ilitumika kama hela. Dhahabu na Chumvi vyote vilikuwa na thamani sawa. Neno ‘salary’ (mshahara) linatokana na neno ‘salt’ (chumvi). Hapa kwetu Tanzania, watu hutumia msemo, ‘Nimekula chumvi nyingi’ kumaanisha kuishi miaka mingi. Katika siku hizo za kale, chumvi ilitumika pia kuhifadhia vyakula. Siku hizi tunatumia rifrijereta, kwa hiyo chumvi chache inahitajiwa isipokuwa kwa matumizi machache ya kusokote

FAIDA YA TANGAWIZI (GINGER)

Image
Tangawizi hutibu magonjwa 72 Tangawizi (Ginger): Tangawizi ni nini? Tangawizi ni kiungo ambacho kinatokana na mizizi ya mmea wa Tangawizi. Mmea huu unafanana sana na Binzari ikiwa bado haijamenywa maganda yake. Na kwa hapa Tanzania Tangawizi hulimwa sana mikoa ya nyanda za juu Kusini na baadhi ya mikoa kama Kilimanjaro, baadhi ya maeneo ya mkoa wa Manyara, Morogoro, na kwingineko nchini. Pia kama bidhaa inapatikana nchi nzima kwa bei nafuu kabisa na kila mtu mwenye uwezo wowote wa kiuchumi anaweza kununua aidha kwa kipande kimoja, fungu au kwa kilo pia. Tangawizi inatumikaje?: Mmea huu unaweza kuonekana kama mmea wa kawaida na watu kuutumia tu kama mazoea lakini Kiungo hiki kinaweza kutumiwa kama Dawa. Kiungo hiki huweza kutumika kikiwa kibichi au kikiwa kimekaushwa na kutengenezwa unga. Nini Faida ya Tangawizi? Tangawizi ni mmea kati ya mimea mingi yenye maajabu, Mmea huu unaweza kutumika kama dawa na kutibu magonjwa mengi tu zaidi ya 72 yaliyo ndani ya miili yetu na kut

faida za embe

Image
Zijue faida za tunda aina ya embe. EMBE ni tunda la mwembe ambao ni mti wenye ukubwa wa wastani una rangi ya kijani kibichi kila wakati. Kabla ya kuzaliwa embe mti huu huwa na maua ya rangi ya waridi hadi nyeupe katika vishada vya maua na msimu wake ni kati ya Desemba hadi Aprili. Tunda la embe umbo lake hutofautiana, mengi yao huwa aidha na rangi ya kijani, manjano ama nyekundu. Embe inaweza kuiva ikiwa mtini lakini ili kuzuia uharibifu kutoka kwa ndege na popo ambao hula tunda hili, wakulima huamua huvuna mara tu inapokomaa kwa kuangusha ikiwa bado haijaiva. Utagundua kuwa embe imekomaa kwa kuiangalia rangi kwani hubadilika kutoka rangi ya kijani hadi ya manjano au nyekundu. Kuna aina nyingi za embe kama vile embe dodo, embe mali, embe bolibo, embe nuka, embe kidney, embe Julie Manzano na kadhalika. Watu wengi hupenda kula embe ikiwa imeiva lakini ulaji wake ikiwa bado mbichi ni jambo muhimu sana kiafya. Nyama ya tunda hili ni tamu pia ina virutubisho kwani ni chanzo ch

FAIDA 13 ZA MACHUNGWA

Image
                      FAIDA 13 YA MACHUNGWA Ni msimu mwingine wa machungwa, yamejaa tele kila kona. Shilingi 100 tu unapata chungwa. Lakini siyo ajabu kama kuna watu msimu unaisha hawajala hata chungwa moja, wala suala la matunda halipo kabisa katika orodha ya milo yao! Inawezekana pia hata kwa wale wanaokula, japo kidogo, hula kama kiburudisho tu bila kujua faida zake mwilini. Katika makala ya leo nitakujuza faida 13 unazoweza kuzipata unapokula chungwa, ambalo limesheheni virutubisho kibao. Kumbuka kuwa hata chungwa moja tu ukila lina kidhi yale mahitaji muhimu ya mwili ya kila siku (daily requirement), iwe chungwa lenyewe au juisi yake halisi. 1. UKOSEFU WA CHOO Kutokana kuwa na kiwango kikubwa cha kirutubisho aina ya kambalishe (fibre), chungwa husaidia usagaji wa chakula tumbuni na hutoa ahueni kwa mtu mwenye matatizo ya ukosefu wa choo. Aidha, kambalishe huondoa kolestro na huimarisha kiwango cha suk

MAANA YA DIVAI

Image
KUNA MADA HUMU INAENDELEA NAMI SIWEZI KUKAA KIMYA WAKATI WATU WANAWEZA POTEZWA,,,,,,,,!!! NAONGELEA KUHUSU KUNYWA POMBE AU DIVAI,,,,,!!! NIVIZURI UNAPOSOMA MAANDIKO UJUE TAMADUNI ZA WAKATI ULE MAANDIKO YALIPOANDIKWA NA TAMADUNI ZA WAKATI HUUU NA MAANA YA NENO LENYEWE DIVAI LINAMAANA GANI,,,!!!! NAANZA NA NENO DIVAI,!!!!! Neno DIVAI LIMETOKANA NA NENO LA KIGIRIKI LINALOITWA IGNIOS,,,,!! MAANA YA NE NO HILI KULE ISRAEL LINAMAANA YA DIVAI PIA ILA SASA TUNATOFAUTIANA MTAZAMO!!!!! LABDA NIKUFAHAMISHE KWA MFANO HUU NDIO UTAELEWA,,,, UKIWEKA,, SODA,, BIA,, REDBULL,, MALTA,, FANTA,, SPRITE,, NDOVU,, KILIMANJARO ,, ZOTE HIZI KWA PAMOJA KULE ISRAEL NI DIVAI SASA LINAKUJA WEWE UNATAKA DIVAI GANI,, MAANA HATA FANTA NI DIVAI,, HATA,, MALTA NI DIVAI,, NDIO MAANA KUNA DIVAI ILIYOCHACHUKA NA DIVAI ISIYOCHACHUKA,,, KWA HIYO MATUMIZI YA HILI NENO DIVAI KWETU HUKU NI POMBE ,,, ILA MFANO MWINGINE NI SAWA KUSEMA  SHAMPENI YENYE KILEVI NA ISIYO NA KILEVI ,,ZOTE NI SHAMPENI ,,, SASA UKIWA I